Monday 24 January 2011

CULTURE YAPATA VIONGOZI WAPYA

 Culture yapata viongozi wapya

Na Salum Vuai

KLABU ya muziki ya taarab na maigizo Culture. Imepata viongozi watakaiongoza kwa kipibndi cha miaka mitatu ijayo.

Hatua hiyo imekuja kutokana na uchaguzi mkuu wa klabu hiyo kongwe nchini uliofanyika Januari 23, kwenye makao yake makuu yaliyopo Vuga m,mjini Zanzibar.

Katika uchaguzi huo uliotanguliwa na mkutano mkuu ambao ulipokea ripoti ya utendaji wa klabu hiyo kwa kipindi kilichopita, Khamis Mikidadi Ali alichaguliwa tena kuwa Mwenyekiti, huku nafasi ya Msaidizi Mwenyekiti ikienda kwa Said Mwinyi Chande.

Taimour Rukuni Taha, alifanikiwa kushika tena nafasi ya Katibu Mkuu, ambapo msaidizi wake anakuwa Hassan Suleiman ‘Chita’ ambaye pia anavaa kofia ya ukatibu mwenezi.

Wengine waliochaguliwa kuongoza kl;abu hiyo na nafasi zao zikiwa kwenye mabano ni pamoja na Chimbeni Kheri Chimbeni (Mshika Fedha), Masoud Mohammed Masoud (Msaidizi Mshika Fedha), Ali Hassan Ali (Mkurugenzi Muzeka) na msaidizi wake anakuwa Juma Abdallah Othman.

Katika safu hiyo ya uongozi pia wamo Makame Kombo (Mkuu wa Michezo), Haaji Nahoda (Mkuu wa Jumba), na wajumbe wawili wa Halmashauri Kuu ambao ni Ali Mrisho Mkanga pamoja na Mtumwa Mbarouk Mamboka.

Viongozi wote hao walitoa ahadi ya kusimamia vyema utekelezaji wa maazimio yaliyomo kwenye mpango kazi wa klabu hiyo kwa kipindi kijacho, na kurekebisha kasoro mbalimbali za kiutendaji zilizojitokeza kabla kwa lengo la kuiimarisha klabu hiyo iliyoasisiwa mwaka 1965.

No comments:

Post a Comment