Monday 24 January 2011

WATOTO WA DK. SHEIN WANGA'ARA MAKUNDUCHI

Watoto wa Dk. Shein wang’ara Makunduchi

Na Mwajuma Juma

TIMU ya soka ya Ofisi ya Rais, Ikulu, juzi iliwatoa nishai wenyeji wao Jamhuri ya Makunduchi, kwa kuichakaza mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa huko Makunduchi.

Katika pambano hilo ambapo watoto wa Dk. Shein walitawala kwa muda wote, walipata mabao yao kupitia kwa wachezeji Makame aliyefunga magoli mawili pamoja na Omar Himid.

Katika mchezo mwengine wa kirafiki, timu ya soka ya Zanzibar Veterans, iliiadhibu bila huruma Baja Veterans kwa kuibanjua mabao 5-1, kipute kilichopigwa uwanja wa Amaan nje.

Mabao ya washindi katika mtanange huo, yalifungwa na Ali Abdallah, Hakim Mohammed, Nassor Mwinyi ‘Bwanga’ na Suluhu Hassan, wakati lile la kufutia machozi kwa Baja lilinasishwa kimiani na Abeid Jiwe.

Michezo yote hiyo ilichezwa kwa lengo la kudumisha urafiki kati ya timu

No comments:

Post a Comment