Tuesday 25 January 2011

DIWANI FUONI AWAONYA WANAOCHAFUA MAZINGIRA.

Diwani Fuoni awaonya wanaochafua mazingira

Na Haji Nassor ZJMMC.
Jumatano 26, Januari 2011.

DIWANI wa wadi ya Fuoni, Wilaya ya Magharibi Unguja, Shaka Hamdu Shaka, amelaani tabia inayofanywa na baadhi ya wananchi hapa Zanzibar ya uchafuzi na uharibifu mazingira ikiwa ni pamoja na ukataji miti, uchimbaji mchanga, mawe na ujenzi holela.

Alisema ni vigumu kwa sasa kurejesha haiba ya visiwani kutokana na jamii kuendelea kufanya uharibifu wa mazingira siku hadi siku.

Akizungumza katika hafla ya kugawa vifaa vya usafi wa mazingira kwa wananachi wa Shehia ya Maungani, Wilaya ya Magharibi jana, Diwani huyo alisema wakati umefika jamii kujikosoa kwa kuchukia aina yoyote ya uharibifu wa mazingira kwa vile ni hatari kwa mendeleo.

Hivyo, aliwashauri wananchi kuhakikisha wanayatunza na kuyadumisha mazingira yanayowazunguuka, ili kizazi kijacho kirithi haiba nzuri yenye vivutio kama ambavyo ilikuwa katika miaka iliyopita.

Alisema uhifadhi wa mazingira hauhusishi taasisi maalum lakini ni jukukumu la watu wote kwa sababu hali ikiwa mbaya itamuathiri kila mtu.

Katika hatua nyengine, Diwani huyo aliwashauri wananchi wa wadi yake kuhakikisha hawawapi nafasi wananchi wakorofi wanaotupa taka ovyo pamoja na kutohifadhi umwagaji maji mitaani.

Alibainisha kwa kusema hilo likiachiwa kuchukua nafasi basi hali itakuwa mbaya wakati wowote mvua zitakaponyesha na kuiathiri jamii kwa kuzuka maradhi ya miripuko.

Aidha aliwasifu wananchi wa wadi ya Maungani kutokana na uamuzi wao wakufanyakazi pamoja kwa kupambana na uchafuzi wa mazingira.

Alifafanua kua kikundi hicho bila ya nguvu za wanashehia wenzao hakitoweza kufikia malengo yao ambapo Diwani huyo katika kuhakikisha Maungani inadhibiti suala la usafi wa mazaingira pia alikabidhi mifuko mitano ya saruji ili kuendeleza ''dampo'' kuhifadhia taka.

Pia alikabidhi vifaa mbali mbali vya usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na mabero, slesha, majembe, mapanga, reki ambapo vifaa hivyo pamoja na saruji vinathamani zaidi ya shilingi 700,000 na kuahidi kuchangia kifedha hali itakaporuhusu.

No comments:

Post a Comment