Tuesday 25 January 2011

DK.SHEIN ATEUA WAKURUGENZI, MAKAMISHNA WAPYA.

Dk. Shein ateua Wakurugenzi, Makamishna wapya

Na Mwandishi Wetu
Jumatano 26, Januari 2011

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein jana amefanya uteuzi wa wakuu wa taasisi mbali mbali serikalini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, iliezea kuwa uteuzi wa watendaji hao umeanza rasmi jana.

Walioteuliwa katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Mkurugenzi Idara Mipango, Sera na Utafiti, Fauzia Mwita Haji, Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji na Utumishi Is-hak Ali Bakari, huku Sheha Mjaja Juma akiteuliwa kuwa Mkurugenzi Idara ya Mazingira.

Wengine ni Mkurugenzi Idara ya Watu Wenye Ulemavu, Abeida Rashid Abdulla, ambapo Dk. Omar Makame Shauri anakuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya UKIMWI na Fatma Mohammed Omar anakuwa Ofisa Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Pemba.

Katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mkurugenzi wa Idara ya Mipango Sera na Utafiti ni Khatib Said Khatib, huku Hassan Khatib Hassan akiteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ni Ahmada Kassim Haji, huku Issa Ibrahim Mahmoud akiteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa.

Wengine ni Ali Juma Hamad anakuwa Mkurugenzi wa Idara ya Maafa, ambapo Iddi Suleiman Suweid anakuwa Mkurugenzi wa Idara ya Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali.

Ofisa Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba ni Amran Massoud Amran.

Katika Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo), aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Sera na Utafiti ni Idrissa Abeid Shamte, ambapo Ramadhan Senga Salmin ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi.

Omar Hassan Omar ameteuliwa kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali, ambapo Msaidizi Mhasibu Mkuu wa Serikali ni Mwanahija Almasi Ali.

Rais pia amemteua Khatib Mwadini Khatib kuwa Kamishna wa Bajeti, ambapo Said Mohammed Hussein ameteuliwa kuwa Kamishna wa Uhakiki Mali na Mitaji ya Umma.

Aidha Saada Mkuya Salum ameteuliwa kuwa Kamishna wa Fedha za Nje ambapo Mkurugenzi wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dar es Salaam ni Shumbana Ramadhan Taufiq, ambapo Ofisa Mdhamini Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo Pemba ni Bakari Haji Bakari.

Rais pia amefanya Uteuzi katika Tume ya Mipango ambapo Ahmed Makame Haji ameteuliwa kuwa Kamishna wa Mipango ya Kitaifa, Maendeleo ya Kisekta na Kupunguza Umasikini.

Kamishna wa Ukuzaji Uchumi, aliyeteuliwa ni Mwita Mgeni Mwita ambapo Seif Shaaban Mwinyi ameteuliwa kuwa Kamishna wa Mipango na Maendeleo ya Watenda Kazi.

No comments:

Post a Comment