Monday 24 January 2011

UWANJA WA MAO TSETUNG KUFANYIWA MATENGENEZO.

 Mao Tsetung kufanyiwa matengenezo

Na Aboud Mahmoud

UONGOZI uliochaguliwa hivi karibuni kusimamia uwanja wa michezo wa Mao Tsetung, umesema unakusudia kuufanyia matengenezo uwanja huo katika sehemu zote muhimu.

Msaidizi Meneja wa uwanja huo Abdullah Thabit 'Dula Sunday', amesema kwa kushirikiana na Meneja wake Hassan Abdulnabi ‘Teso’, watahakikisha kazi hiyo inafanyika kwa ufanisi mkubwa.

Maeneo aliyoyataja kuwa yatapewa kipaumbele, ni pamoja na ujenzi wa choo uwanjani hapo.

"Kuna sehemu nyingi zinazohitaji kufanyiwa matengenezo katika uwanja huu, kuna mambo mengi muhimu kuwemo katia uwanja wa michezo kwa mfano vyumba vya kubadilishia nguo kwa wanamichezo, waamuzi na kadhalika”, alisema.

Hata hivyo, hakueleza ni wapi wanatarajia kupata fedha kwa ajili ya kazi hiyo, wala kutoa muda wa kufanyika na kumalizika kwake.

Uwanja huo uliojengwa kwenye miaka ya mwishoni mwa 40 na mwanzoni mwa 50, una historia kubwa hapa nchini ambapo uliwahi kutumika kwa mashindano ya Gossage, na sasa unakabiliwa na hali mbaya kila eneo.

Licha ya uchakavu na kuporomoka kwa baadhi ya kuta zake, uwanja wa Mao Tsetung ndio unaotegemewa sana kwa michezo mbalimbali ikiwemo ligi kuu ya soka ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment