Monday 23 May 2011

AMEIR AMPANIA RAZA KATIKA KONGAMANO

Ameir ampania Raza katika kongamano

Asema halitakuwa la watu wasiojua soka
Na Donisya Thomas
LICHA ya wadau wataotaka kushiriki kongamano la soka linaloandaliwa na Makamu wa Rais wa ZFA Unguja, Haji Ameir kutakiwa kujaza fomu za ushiriki, mfanyabiashara Mohammed Raza atapewa mwaliko maalumu ili afahamishwe kuwa ZFA ni chama cha soka na sio cha siasa.
Makamu huyo wa Rais, amesema kongamano la wadau wa soka Zanzibar litafanyika mwishoni mwa mwezi ujao, ambapo ameonesha kukerwa na kauli ya Raza aliyoitoa hivi karibuni, kuwataka wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho kuzingatia maslahi ya umma na sio ya wagombea au utashi binafsi.
Ameir amemwambia mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Bwawani, kuwa kongamano hilo linaloandaliwa kujadili changamoto mbalimbali zihusuzo soka la Zanzibar na namna ya kuzipatia ufumbuzi, linapangwa kufanyika katika ukumbi wa Salama hoteli ya Bwawani.
Alisema kongamano hilo litawashirikisha wadau wa mchezo huo nchini kutoka makundi tafauti ikiwa pamoja na wachezaji wa zamani wakiwemo waliochezea timu za taifa za Zanzibar na Tanzania, sambamba na waandishi wa habari za michezo.
Mbali na hao, Makamu huyo alisema pia wanasheria, watu waliowahi kuiongoza ZFA kwa vipindi tafauti, makocha, waamuzi wa ligi madaraja mbali mbali, wajumbe wa mkutano mkuu wa ZFA na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi watashirikishwa katika kongamano hilo.
Alisema mipango iko mbioni kununua muda katika kituo cha Televisheni Zanzibar, Sauti ya Tanzania Zanzibar, Zenj FM pamoja na Bomba FM, kwa ajili ya kutangaza moja kwa moja kongamano hilo, pamoja na kumualika mmoja wa viongozi wa juu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa mgeni rasmi.
Hata hivyo, Haji Ameir alisema sio kila mtu ataruhusiwa kushiriki kongamano hilo, bali itatolewa fursa kwa watu maalumu hasa wale watakaowahi kuchukua fomu za kushiriki ambao wana uelewa wa mchezo wa mpira wa miguu.
Alisema siku zitakapokaribia fomu za kuomba ushiriki zitatolewa bure kwa muda maalumu, na kwamba ni washiriki waziozidi 200 ndio watakaoruhusiwa kutia mguu katika ukumbi wa Salama ambako kongamano hilo litafanyika, huku gharama zote zikitoka mfukoni mwa Makamu huyo na sio ZFA.
"Sio kila mtu atashiriki kongamano hilo, tutatoa fomu maalumu ili kupata idadi ya washiriki, na tutaanza asubuhi hadi jioni, watakaobakia nyumbani watasikiliza kupitia vyombo vya habari nilivyovitaja, hata Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, wataalikwa kwa idadi maalumu kwa kuangalia wale wenye uelewa wa soka miongoni mwao", alifafanua.
Kongamano hilo linaandaliwa kufuatia hali ya hewa ya soka Zanzibar kutawaliwa na malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali dhidi ya uongozi wa ZFA unaodaiwa kuchangia kuporomosha kiwango cha mchezo huo nchini, na kutakiwa kuachie ngazi

No comments:

Post a Comment