Monday 23 May 2011

TANGA FRESH YAOMBA MSAMAHA WA KODI.

Tanga Fresh yaomba msamaha wa kodi

Na Tumaini Kawogo, Dar
KAMPUNI inayojishughulisha na usindikaji pamoja na uuzaji wa maziwa ya Tanga Fresh Limited, imeitaka serikali iwasaidie kuwafutia kodi ili kukuza uzalishaji wa maziwa hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam ofisa masoko wa kampuni hiyo Chares Benjamin, alisema wamekuwa wakipata faida kidogo kutokana na kodi inayotozwa kuwa kubwa.
Alisema kampuni yao imekuwa ikizalisha bidhaa nyingine kutokana na maziwa fresh ambazo ni yoghurt, samli, jubin, na maziwa ya mtindi lakini pamoja na hilo bado imekuwa ni tatizo katika ukusanyaji mapato.
Aidha alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ambapo moja ya changamoto hizo ni kukwama kwa magari yanayosafirisha bidhaa hizo hasa katika mikoa ya Dodoma, Tanga, na Morogoro ambapo barabara zimekuwa zikiharibika kutokana na mvua nyingi zinazonyesha.
Hata hivyo alisema kuwa wanatarajia kufanya maonyesho ya usindikaji maziwa kwa makampuni 20 ya ndani na nje ya nchi ambapo yatafanyika Mei 25 hadi 27 mwaka huu katika hoteli ya Movenpick.
Aidha aliwataka wananchi kujijengea mazoea ya kunywa maziwa ili kuweza kujenga afya zao hasa kwa watoto wadogo.

No comments:

Post a Comment