Monday 23 May 2011

WANAFUNZI 500 WASHIRIKI ZOEZI LA UPANDAJI MITI

Wanafunzi 500 washiriki zoezi la upandaji miti

Na Suleiman Rashid, Pemba
ZAIDI ya wanafunzi 500 wa skuli mbali mbali kisiwani Pemba wameshiriki katika zoezi la upandaji wamiti kwenye eneo la vilima vitatu Michweni ambayo imeathirika na mazingira.
Mazingira katika eneo hilo yameharibika vibaya kutokana na uchimbwaji wa kifusi na uchongaji wa matufali ya mawe kwa ajili ya ujenzi.
Zoezi hilo la upandaji miti lina lengo la kuadhimisha mwaka wa kujitolea kwa nchi za Umoja wa Ulaya limetayarishwa na Jumuiya ya Global Network of Religion for Children (GNRC).
kwa ajili ya kuyarejesha maeneo hayo yalio athiriwa na uchfuzi wa mazingira kwa kushirikian na jamii kulipanda miti.
Akizungumza wakati wa kulizindua zoezi hilo ofisa wa utumishi wa wilaya Michewni, Hamadi Mbwana Shaame aliiomba Jumuiya ya Ulaya kuendelea kusaidia ili kuyaokoa maeneo mengi ya Micheweni ambayo mazingira yake yameathirika.
Alisema wakati harakati za binaadamu za kujitafutia maisha zikiendelea zimekuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira na kusababisha nchi kupata hasara ya kutumia fedha ili kuyarejesha maeneo hayo katika hali ya kawaida.
“Maeneo mengi ya kisiwa chetu yameharibiwa hasa hapa kwetu Michewni ukataji wa kokoto na mawe umeacha mashimo makubwa”, alisema Shaame.
Kwa upnade wake Haji Vuai Haji kutoka taasisi ya kujitolea, aliwataka wananchi wa Michewni kuitunza miti hiyo ili lengo la kutunza eneo hilo liweze kufikiwa kwa kutoikata ovyo.
Alisema wananchi wa Micheweni wanafaa kuiga mfano wa marehemu Dk. Omar Ali Juma, Makamu wa Rais wa zamani wa Tanzania, ambaye alijishughulisha kikamilifu kuwashajiisha wananchi wa Micheweni kupanda miti.
Kwa upande wake Mwalimu Asha Msabaha akiwakilisha wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali alisema kutoka na mkakati wa utunzaji wa mazingira duniani wananchi wa Micheweni kupunguza ama kuacha kuyachafua mazingiara.

No comments:

Post a Comment