Tuesday 3 May 2011

SINA UTAJIRI WA KUTISHA - RIDHIWANI KIKWETE

Sina utajiri wa kutisha – Ridhiwani Kikwete

Asema wanasiasa wapuuzwe, wanadanganya umma
Na Kunze Mswanyama
WAKILI wa kujitegemea nchini, Ridhiwani Kikwete,amekanusaha tuhuma alizobebeshwa na wanasiasa wawili maarufu kuwa ana utajiri mkubwa kiasi cha kutisha, ilhali ameanza kazi hivi karibuni mara baada ya kumaliza masomo yake Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwanasheria huyo aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa atatoa ushirikiano kwa mtu yeyote atakaye taka kuthibitisha utajiri wake huo, ambapo ilitajwa pia anamiliki vyombo mbalimbali vya usafiri yaliwemo malori, mabasi, majengo makubwa ya kupangisha na kutembelea gari lenye thamani ya shilingi milioni 400.
Alisema wanasiasa hao wanaomtuhumu wanaudanganya na kuuhadaa umma wa Watanzania dhidi ya madai yao hao iliwaamini kuwa ana mali nyingi
Rikadhaniwa zinatokana na nafasi aliyo nayo mzazi wake yaani Jakaya Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa.
"Mimi ni raia wa kawaida, mtanzania na wakili sina kinga za aina yoyote, na ninatambua utawala bora unapoheshimu haki za binadamu. Hivyo natoa rai kwa wazee hawa ambao mimi pia nawaheshimu kuwa watumie vyombo vya habari walivyovitumia ili kutengeneza habari njema na siyo kutafuta sifa za kisiasa au kuonekana wao wanajua sana kuongea,wasiwe makanjanja wa habari",alisema Ridhiwani.
Wakili huyo alisema, "kuwa habari hizi hazikuwa za kweli ni za kizushi, zilizojaa uongo na ambao madhumuni yake nayaona yanalenga kunichafua mimi na wazazi wangu katika umma wa watanzania na kujenga chuki kati yetu na jamii hii”.
Aidha alisema kuwa umma wa watanzania uelewe kuwa hamiliki mali hizo zilizotajwa na kama kuna mtu ana ushahidi autoe ambapo yuko tayari kuwajibika mbele ya umma.
Ridhiwani alisema si mara ya kwanza kwa baadhi ya wanasiasa kutoa taarifa za uongo ambapo mmoja wa wanasiasa hao, aliwahi kusema yeye na vijana wengine 50 walijifungia katika hoteli ya La Cairo iliyopo Mwanza kuharibu uchaguzi wa mwaka jana.
“Pia amewahi kuwaongopea watanzania kuwa kuna makontena ya kura yamekamatwa huko Tunduma Mkoani Mbeya,bila ya aibu Mzee huyu anaudanganya umma huu, hivi tunaweza kweli kuwa na rais muongo na tukaendelea kiuchumi, si atatudanganya hata mambo mengine muhimu?"
Ridhiwani alisemaalitoa rai kwa watanzania kwa kuwataka kutowasikiliza kwani vyanzo vya habari vya wanasiasa hao vinatoa taarifa potofu.

No comments:

Post a Comment