Saturday 14 May 2011

WALIOACHA DAWA ZA KULEVYA WAPEWE TAALUMA

Walioacha dawa za kulevya wapewa taaluma

Na Zainab Jecha, MCC
ZAIDI ya shilingi milioni 12 zimetumika kwa ajili ya mafunzo maalum kwa vijana wa jumuiya inayopambana dhidi ya UKIMWI na dawa za kulevya ya ZAIDA kwa lengo la kutoa elimu ili kupunguza ya maradhi hayo.
Ofisa miradi takwimu na ufuatiliaji wa mradi wa F.H.I family health international, Mbarouk Said Ali alieleza hayo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi.
Alisema elimu iliyotolewa iliwalenga vijana walioacha matumizi ya dawa za kulevya, ili kuwawezesha kutambua athari zinazopatikana dhidi ya utumiaji wa dawa hizo.
Ofisa huyo alisema elimu waliyopatiwa vijana hao pia ililenga kuwapa changamoto vijana hao katika kukabiliana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Akizungumzia changamoto inayoikabili jumuia hiyo, alisema ni pamoja na wafadhili kuchelewesha misaada na kusababisha kuzorota kwa miradi mbali mbali ya jumuiya hiyo.
Ofisa huyo alitoa wito kwa wafadhili mbali mbali kusaisaidia jumuia hiyo kwani imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha tatizo la dawa za kulevya na UKIMWI linamalizika hapa nchini.
Aidha aliwataka vijana kuacha matumizi ya dawa za kulevya na kujishughulisha kazi mbali mbali za ujasiriamali ambazo zitawawezesha kujitegemea na kuondokana na umasikini.

No comments:

Post a Comment