Saturday 14 May 2011

SERIKALI YASHAURIWA KUSHUSHA USHURU WA VIFAA VYA MICHEZO.

Serikali yashauriwa kushusha ushuru wa vifaa vya michezo
Na Mwantanga Ame
SERIKALI imshauriwa kushusha ushuru wa vifaa vya michezo ili kuziwezesha klabu ziliopo wilayani kumudu gharama na kuweza kufanya vizuri katika michuano mbalimbali.
Hayo yalielezwa na Meneja wa uwanja wa Amaan, Khamis Ali Mzee, hivi karibuni.
Alisema, michezo mingi imekuwa ikichezwa zaidi mjini kunakosababishwa na ukosefu wa vifaa jambo ambalo serikali inapaswa kuliangalia suala la kupunguza ushuru ili timu za vijijini ziweze kumudu gharama hizo.
Alisema mchezo wa skwash hivi sasa unawanufaisha zaidi wanamichezo wa mjini kutokana na kuwepo kwa viwanja viwili vinavyotumika kwa mchezo huo wakati vijiji kukiwa hakuna hata kiwanja kimoja.
Meneja huyo alisema kukosekana kwa miundo mbinu hiyo katika vijiji kwa kiasi kikubwa kumewafanya wakaazi wa maeneo hayo kushiriki zaidi katika mchezo mmoja na kupelekea vipaji vyengine kupotea.
Aliutaja mchezo wa mpira wa mikono hivi sasa unachezwa katika vijiji vingi kutokana na kuhamasishwa, lakini mpira wa kuchezea ikiuuzwa kwa shilingi 35,000 hadi 45,000.
Alisema hizo ni gaharama kubwa kwa wananchi wa kijijini kuweza kumudu vifaa vya michezo hivyo ni
vyema serikali ikafikiria kupunguza gharama hizo.

No comments:

Post a Comment