Saturday 14 May 2011

WAWEKEZA WA KIGENI WANYANYASA WABIA WAZALENDO

Wawekezaji wa kigeni wanyanyasa wabia wazalendo

Na Mwantanga Ame
BAADHI ya watendaji serikalini wamedaiwa kuchukua mabilioni ya fedha, kwa kushirikiana na wawekezaji wasio waaminifu na kuwakandamiza wawekezaji wazalendo kuuwa sekta ya utalii.
Hayo yamejitokeza mbele ya Kamati ya Mifugo, Utalii, Uwezeshaji na Habari ya Baraza la Wawakilishi, ilipofanya mazungumzo na baadhi ya wamiliki wa mahoteli ya kitalii huko Marumbi wilaya ya kati Unguja.
Watendaji wa ngazi za juu serikalini hasa sehemu ya mapato wamelalamikiwa na wawekezaji wazalendo wamekuwa wakishirikiana na wawekezaji wa nje na huchukua mabilioni ya fedha kupitia sekta hiyo ya utalii na kuwakandamiza kwa vitisho wazalendo.
Mmoja wa wamiliki hoteli ya kitalii, Ali Mgeni, alisema hali hiyo imejitokeza baada ya kufuatwa na watendaji hao kutakiwa kutohoji juu ya mmoja wa wamiliki aliyeingia naye mkataba kumbaini kwenda kinyume na makubaliano waliyofungiana mkataba wake.
Alisema Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi (ZIPA), imemruhusu Mwekezaji huyo kuzimiliki hoteli tisa zilizomo katika ukanda wa kati na Kaskazini, na huku akiwa hana faida yoyote anayoingiza katika serikali kutokana na kuendeleza utalii kwa njia ya pekeji ambapo watalii hulipia kila kitu nchini kwao.
Alisema alichokibaini Mwekezaji huyo amekuwa akipata nguvu ya kufanya hivyo kutokana na kushirikiana na baadhi ya maafisa wa kodi hapa nchini kwani baadhi yao kumfuata na kumtaka asiliingilie suala hilo.
Alisema kinachomuuma kuona Muwekezaji huyo bado serikali inamfungisha mikataba ya kumiliki hoteli nyengine, wakati wakijua kuwa mikataba yake haina faida na serikali kutokana na watalii anaoleta sio wanakuja kutumia kwa vile tayari wameshalipia kila kitu nchini Italia.
Alisema hali hiyo humfanya alieingia nae ubia kutofaidika kwani hutegemea zaidi kupata fedha za wageni ambao hutumia ziada ya kile walicholipia nchini kwao ambapo kwa mwezi huweza kupata shilingi 200,000.
“Ingawa wageni hao wanakuja katika hoteli na hujazana kwa msimu lakini huwa hawatumii na kama watatumia hawazidi zaidi ya shilingi 200,000 kwa mwezi kwani ile chai yao basi imeshalipiwa nchini Italia sie kazi yetu kumuwekea mgeni anywe” alisema Muwekezaji huyo.
Alisema hapo awali yeye aliingia ubia na Muwekezaji huyo kwa kutomudu gharama za ujenzi kwa kutumia kiwanja chake kwa kushirikiana na kaka yake, lakini kaka yake huyo anaeishi Italia hivi sasa anashindwa kumfahamu kwa vile hapati shauri jema kutokana yeye ndie aliehusika kumleta mwekezaji huo.
Alisema cha kushangaza mmiliki huyo, hivi sasa amebadilisha hata makubaliano ya mwanzo ambapo alitakiwa kuilipa familia hiyo asilimia 25 lakini amebadili mkataba wake na kumueleza hivi sasa asilimia anayotakiwa kuipata ni 15 lakini hata hivyo hivi sasa hawaipati na anapojaribu kumuuliza kaka yake humwambia atalipiwa na Mungu.
Mmiliki huyo alisema Hoteli ambazo Mwekezaji huyo amezichukua ni zile ambazo zilianzishwa kwa mfumo wa Uwekezaji wa pakeji na wawekezaji wake kushindwa kuziendesha ambapo yeye huzinunua kwa Wawekezaji wenzake nchini kwao na kukubaliwa kuwekeza kama mmiliki halali kutoka kwa wenzake hao.
Akiendelea alisema hali hiyo imekuwa ikimfanya kukabiliwa na madeni mengi ya wasambazaji wa huduma katika hoteli hiyo ambapo zimefikia zaidi ya shilingi milioni 41 na baada ya kumtumia taarifa za madeni Mbia mwenzake amemleta shilingi milioni 23 huku kukiwa na bakaa ya madeni.
Kuhusu malipo ya wafanyakazi nayo alisema hivi sasa kutokana na msimu kuwa mdogo amekubaliana na baadhi ya wafanyakazi kupumzika hadi msimu utapoanza, lakini kwa waliobakia bado ameshindwa kuwalipa mshahara wao wa mwezi uliopita.
Kuhusu malipo ya kodi za serikali alisema hizo hazina mashaka kutokana na Muwekezaji huyo amekuwa akijitahidi kulipia kodi zote anazotakiwa kuzilipa serikalini.
Mwekezaji huyo alisema hivi sasa anajitayarisha kutafuta mwanasheria ikiwa ni hatua ya kuanza maandalizi ya kumfikisha mbia mwezake Mahakamani kwa kushindwa kumpatia sehemu ya asilimia aliyotakiwa kuipata kulingana na mkataba waliokubaliana.
Hapo awali alisema katika makubaliano yao walikubaliana fedha za majengo wajilipe ndani ya kipindi cha miaka minne lakini cha kushangaza imefikia miaka sita hawajaanza kupata asilimia yao ya miaka miwili na badala yake ameletewa mkataba mwengine unaopunguza asilimia zake.
Mkurugezi Mipango katika Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Ashura Haji Mrisho, alisema matatizo ya aina hiyo yapo mengi kutokana na baadhi ya wananchi kuamua kushirikiana na wawekezaji kwa kuwapa ardhi ili wajenge bila ya kupitisha miradi yao ZIPA.
Alisema Wananchi wa maeneo ya ukanda wa bahari huingia mikataba kwa kushea ili wajengewe kwa njia ya kuendesha hoteli hizo jambo ambalo huwasababishia matatizo baadae kutokana na baadhi ya wanaoshirikiana kutokuwa waaminifu na hukatisha mikataba ya Wazalendo ama huwafikisha mahakamani pale wanapoonesha nia ya kutaka kujitoa katika miradi walioanzisha.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Asha Bakari Makame, alisema ipo haja kwa watendaji wa Wizara hiyo kuyaona matatizo ya aina hiyo kwani serikali imekuwa inakosa mapato mengi huku watu wachache wakifaidika na miradi ya aina hiyo.
Alisema, utalii wa aina hiyo, hivi sasa unaonekana haufai na haelewi kwanini ZIPA na Idara nyengine zinazosimamia sekta hiyo kuendelea kuwafungisha mikataba wawekezaji wanaotaka kuendesha utalii kwa mbinu ya pakeji.
Mwenyekiti huyo aliwataka viongozi wa Wizara hiyo kukaa pamoja na ZIPA, ZRB, na wadau wengine kulizungumzia suala hilo na kuliandalia mkakakati maalum huku wakitaka kufanyika uchunguzi kuona wadau hao kama hawana mkono wao wa kuifilisi serikali kwa kushirikiana na wawekezaji hao.
Alisema hilo ni vyema wakalishughulikia kwani linaweza kuwafanya wazanzibari wakajikuta ardhi yote imechukuliwa na wageni kutoka na kuingia nao ubia watapojaribu kufuta mikataba watapandishwa mahakamani na kushindwa kulipa fedha watazokuwa wanadai.
Akitoa maelezo yake Katibu Mkuu wa Wizara ya habari Utamaduni, Utalii na Michezo, Dk.Ali Mwinyikai, alisema atahakikisha wanalifanyia kazi suala hilo ikiwa pamoja na kuwapatia zaidi elimu wawekezaji wazalendo kufahamu haki zao na namna ya kuingia mikataba kwa kutumia njia ya kodi badala ya kukubali ubia nao.
Ni hivi karibuni tu Baraza la Wawakilishi lilipokea ripoti ya

No comments:

Post a Comment