Tuesday 17 May 2011

WAUMINI WAGHADHIBISHWA NA PADRI KUMCHAPA MAKOFI MUUMINII

Waumini waghadhibishwa Padri kumchapa makofi muumini

Na Kunze Mswanyama, Kigoma
WAUMINI wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Gungu Mkoani Kigoma, wamekilaani kitendo cha aibu cha Padri Sabasi kumtandika makofi kanisani muumini wake.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, waumini hao walisema kitendo kilichofanywa na Padri huyo ni cha aibu na kinapaswa kulaaniwa.
“Kutokana na uzee wake mama yetu aliyepigwa makofi kweli kitendo hicho kimetushusha mori kwenda kuabudu kanisani hapo, viongozi wa dini wanaongozwa na roho wa upole sijui huyu anaongozwa na roho gani hiyo", alisema mmoja wa waumini hao, John Xveri.
Mama aliyepigwa makofi na Padri inasemakana ana umri wa miaka 76 na alipigwa baada ya kupokea mkate wa sakramenti na kisha kukaa kwenye kiti badala ya kusimama ili kusubiri kuutumia pamoja na wenzake,jambo lililomkera padri huyo hivyo kumchapa vibao ajuza huyo.
Kwa ukali kabisa kabla ya kushusha kipigo, alisema “Kwa nini unakula sakramenti hali umekaa chini, hujui kama ni dhambi?” alisema Padri huyo.
Xveri alisema wakati Pdri huyo kutoa ukali huo walidhani ni sehemu ya kupata upole wa Yesu na pia huruma zake, lakini wanakutana na yale yale ya duniani ambayo kamwe hayaelezeki.
Alipoulizwa juu ya kitendo hicho cha kumpiga kondoo wake, Padri Sabasi alisema kuwa kwa taratibu za kanisa lao hutakiwa kusimama kwenye foleni ukiwa na mkate huo hadi pale utakapoamriwa kuitumia.
Alisema mama huyo alichukua mkate huo mtakatifu na kuuweka kwenye maziwa yake kisha kukaa mimi nikajua anataka kuufanyia mambo ya kishirikina.
Kutokana na hali hiyo waumini wapatao 2,000 wamedhamiria kutokwenda kusali kanisani hapo wanatakiwa wauone upendo wa Mungu na badala yake wanakutana na kadhia za ajabu kama hiyo ambayo hadi sasa Baraza la wazee wa Kanisa hilo wanakutana ili kuchukua hatua dhidi ya Padri huyo.

No comments:

Post a Comment