Monday 23 May 2011

MIEMBEZI DUMA HAKUNA MBABE.

Miembeni, Duma hakuna mbabe

Na Mwajuma Juma
TIMU za Miembeni na Duma, zimelazimika kumaliza dakika 90 kwa sare ya 0-0 katika pambano la ligi ndogo lililochezwa kwenye uwanja wa Mao Dzedong ,mwishoni mwa wiki.
Kwa matokeo hayo, Miemveni imepanda hadi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 12, ikitanguliwa na Mafunzo inayoongoza lig hiyo kwa pointi 14 sawa na Jamhuri ikishika nafasi ya pili kwa tafauti ya magoli ya kufunga na kufungwa kati yake na askari hao wa wafungwa.
NAYE SULEIMAN BANGAYA, anaripoti kuwa timu kongwe ya soka Zanzibar, Kikwajuni, imeikong'ota Mlandege bila huruma kwa kuibugiza magoli 4-1 katika mchezo wa ligi daraja la kwanza Taifa.
Na katika mchezo mwengine wa ligi hiyo, timu ya Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) na Chwaka, zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka uwanjani kwa sare ya bao 1-1 kwenye uwanja wa Fuoni.
Nayo ligi daraja la pili Wilaya ya Mjini, mchezo uliochezwa uwanja wa Dimani, ulishuhudia watoa pasipoti Uhamiaji wakila sahani moja na Coast Stars kwa sare isiyokuwa na magoli, huku Mwembeshauri ikiichakachua Mwembeladu kwa kipigo cha 4-1.
Matokeo ya Central katika viwanja tafauti yanaonesha Amani Kids 3, Valencia 1, Arizona 8, Darajabovu 1, na Kwahani 4, Beach Boys 1.

No comments:

Post a Comment