Monday 23 May 2011

WAKULIMA WATAKIWA KUACHA KUUZA MAZOA MASHAMBANI.

Wakulima watakiwa kuacha kuuza mazao shambani

Na Jumbe Ismailly, Manyoni
KATIBU wa uchumi na fedha CCM Taifa, Lameck Nchemba Mwigulu amepiga marufuku tabia ya baadhi ya wakulima wilayani Manyoni, kuuza mazao yakiwa bado shambani.
Mwigulu alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye mji mdogo wa Itigi, wilayani Manyoni wakati akizungumza na wanachama wa CCM wa kata za Itigi na Majengo kwenye sherehe za ushindi wa kesi ya uchaguzi iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa jimbo la Manyoni Magharibi, John Paulo Lwanji.
Alisema tabia ya kuuza chakula kikiwa shambani ni hatari na inaweza kuwaweka wananchi kwenye hali ya njaa, badala yake aliwataka wayatunze ili yaweze kuwasaidia wakati wa matatizo.
“Wana Manyoni magharibi mna bahati sana hata wakati wa hali ya hewa ilipokuwa mbaya, niliwakuta mna ufadhali kuliko sehemu zingine, kwa hiyo chakula matakachovuna nawaombeni mkitunze na msiuze kikiwa shambani”, alisema.
Akizungumzia kuhusu chama, Mbunge huyo alisema mshikamano unahitajika na kuwakumbusha wanachama wa chama hicho juu ya wajibu na umuhimu wa mshikamano ndio siri ya katika upatikanaji wa maendeleo.
Katibu huyo wa uchumi na fedha hakusita kuwashauri baadhi ya wanachama wa chama hicho walioanza kupotoshwa warejeshe akili zao kwenye mshikamano ili mafanikio zaidi yaweze kupatikana.

No comments:

Post a Comment