Tuesday 17 May 2011

KOROSHO YAPELEKA NEEMA MKURANGA

Korosho yapeleka neema Mkuranga

Na Shan Hussein, Mkuranga
HALMASHAURI ya wilaya ya Mkuranga, Mkoani Pwani, imefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 11 katika msimu wa mwaka jana wa zao la korosho.
Mkuu wa wilaya hiyo, Henry Clence, alitoa taarifa hiyo katika Kikao cha Madiwani, kilichokuwa kikijadili maendeleo ya halmashauri hiyo, na kutoa taarifa juu ya fedha zilizopatikana katika zao hilo.
"Miaka ya nyuma tulikuwa tukipata mapato kidogo katika zao hili, baada ya serikali kuweka mfumo wa sitakabadhi ghalani, zoezi hili linakwenda vizuri na kusababisha wilaya kupata fedha nyingi na wakulima kunufaika na zao hilo,''alisema.
Mkuu huyo alisema miaka ya nyuma kilo moja ya korosho, ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi 150, lakini baada ya mfumo kuanza wa stakabadhi ghalani kilo moja ya korosho imeuzwa mpaka shilingi 1,800.
Alisema kupatikana kwa fedha nyingi kumesaidia kupatiwa pembejeo ya ruzuku nyingi ambayo thamani yake ni shilingi milioni 43, hivyo itawasaidia wakulima katika kuongeza uzalishaji wa korosho, ikiwamo na kupulizia mashamba yao kwa wakati.
Clemence aliwataka madiwani kuwahamasisha wakulima kupalilia mikorosho yao kutokana na hivi sasa kuwa na korosho nyingi, pamoja na kupulizia dawa.
"Mpande na miembe ya miaka michache ipo mingi tu, pale mnapo vuna korosho zenu msikae bure na baadaye anaanza tena kunufaika na zao la miembe,''alisema, mkuu huyo.
Aliongeza kuwa, mikorosho sasa hivi imekuwa na soko kubwa Kutokana na kusimamiwa kikamilifu, pia alisema taarifa kutoka soko la juu inasema kuwa korosho za Mkuranga ni tamu kuliko korosho za maeneo mengine.

No comments:

Post a Comment