Thursday 23 June 2011

FAINI YAIPONZA AMANI FRESH.

Faini yaiponza Amani Fresh

Na Mwajuma Juma
CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA) Wilaya ya Mjini, kimeipa ushindi wa bure timu ya Enugu kufuatia hatua ya kuzuiwa wapinzani wao Amani Fresh kwa kushindwa kulipa faini iliyopigwa na chama hicho.
Amani Fresh inayoshiriki ligi daraja la pili hatua ya 12 bora, ilitakiwa kulipa faini ya shilingi 50,000, baada ya kubainika kufanya vurugu siku ilipocheza na timu ya Jang’ombe Boys mara baada ya kumalizika kwa mchezo.
Kwa mujibu wa Katibu Msaidizi wa chama hicho Omar Mohammed, timu hiyo ilifanya vurugu Juni 18, mwaka huu katika uwanja wa Mao Dzedong kwa kuwashambulia waamuzi pamoja na kamisaa wa mchezo, ambapo ilifungwa bao 1-0.
Enugu na Amani Fresh zilipangwa kucheza juzi saa 8:00 mchana katika uwanja wa KMKM Maisara, kabla kuzuiliwa na ushindi kupewa wapinzani wao.
Mbali na mchezo huo, wakati wa saa 10:00 timu za Kilimani na Mwembeshauri zilichuana na Kilimani ikakala kwa bao 1-0, huku katika dimba la Mao Dzedong wakati wa saa 8:00 mchana, Jang’ombe Boys ikaifunga Red Stars bao 1-0.

No comments:

Post a Comment