Thursday 23 June 2011

SI KAZI YA TFF, ZFA KUCHAGUA WACHEZAJI TAIFA STARS.

Si kazi ya TFF, ZFA kuchagua wachezaji Taifa Stars

Na Madina Issa
SHIRIKISHO la Soka Tanzania 'TFF' na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), havina jukumu la kuchagua wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'.
Akijibu suala la Mwakilishi wa nafasi maalumu wanawake, Viwe Khamis Abdallah katika kikao cha Baraza la Wawakilishi jana, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii, na Michezo Bihindi Hamad Khamis, alisema jukumu hilo ni la kocha mkuu aliyepewa dhamana ya kuinoa timu hiyo.
Katika suala lake la nyongeza, Mwakilishi huyo alitaka kujua ni wachezaji wangapi waliochaguliwa kutoka Zanzibar kuchezea timu hiyo.
Akijibu, Naibu Waziri huyo alisema wachezaji wa Zanzibar waliomo kwenye kikosi cha timu hiyo sasa ni wanne.
"Ukweli ni kwamba vyombo hivi TFF na ZFA huwa havikai pamoja katika kutayarisha timu ya tafa ya Tanzania, kwa vile jukumu hilo ni la kocha aliyepewa dhamana ya kufundisha timu hiyo" alisema Bihindi.
Naye Waziri wa Wizara hiyo Abdilahi Jihad Hassan, alitoa ufafanuzi kuhusu msaidizi wa kocha mkuu kwa kusema, kocha huyo pia ndiye anayeamua na kuagiza ni nnai awe masidizi wake bia kuangalia upande anaotoka.
Jihad alitoa ufafanuzi huo kufuata suala la Mwakilishi wa jimbo la Rahale Nassor Salum Ali 'Jazeera', aliyehoji kwa nini utaratibu wa kugawana nafasi za ukocha kati ya pande mbili za muungano haufuatwi sasa.
Mapema, Mwakilishi huyo alisema siku za nyuma, Taifa Stars iliundwa na makocha kutoka nchi mbili huku upande mmoja ukitoa kocha mkuu na mwengine msaidizi wake

No comments:

Post a Comment