Tuesday 21 June 2011

NEW GENERATION QUEENS ZIARANI MOSHI.

New Generation Queens ziarani Moshi

Na Khamis Amani
TIMU ya soka la wanawake New Generation Queens, iko mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, kwa ajili ya kushiriki mashindano ya CHRISS yanayoshirikisha timu za Afrika ya Mashariki na Kati.
Wanasoka hao 16 na viongozi wao, wanashiriki michuano hiyo iliyoanza jana Moshi, chini ya udhamini wa Jumuiya ya Kikristo duniani.
Kwa mujibu wa Meneja wa timu hiyo Salum Jenga Simba, timu yake imeondoka na kikosi kamili kitakachoweza kutoa ushindani mkubwa kwa wapinzani wao watakaopangiwa, kwa lengo la kujihakikishia ushindi wa ngarambe hizo.
"Ni faraja kubwa kwetu, kwani haya ni mashindano yetu ya kwanza tokea kuanzishwa kwa timu yetu, naamini ni fursa pekee ya kuitangaza kisoka timu yetu katika ramani ya Afrika Mashariki na Kati pamoja na duniani kwa ujumla", alisema Salum Jenga.
Hivyo amewahakikishia wapenzi wake kutokuwa wasiwasi juu ya vijana wao hao, ambao wameondoka wakiwa kamili kamili kukabiliana na upinzani wowote utakaowakabili kwa lengo kujinyakulia ushindi.

No comments:

Post a Comment