Tuesday 21 June 2011

MPAKA VINYESI SKULI MBARONI

Mpaka vinyesi skuli mbaroni
• Asema wako kundi lililopangwa ‘shifti’
• Yahusishwa na ushirikina
Na Ameir Khalid
HATIMAE wananachi wa kijiji cha Muungoni Wilaya ya Kusini Unguja wamefanikiwa kimtia mikononi mtu anaedaiwa kupaka kinyesi skuli ya msingi Muungoni kwa muda mrefu katika mazingira ya kutatanisha.
Kazi hiyo ya kukamata mtu huyo haikuwa rahisi baada ya kuhangaika kwa kipindi kirefu ambali limekuwa likihusihwa na masuala ya uchawi na iliwalazimu kutumia kila mbinu ili kufanikisha lengo hilo na hapo jana limetimia.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika eneo la tukio mmoja ya wanakijiji hao ambaye ndiye hasa aliyemkamata mtu huyo, Mohamed Busra alieleza mkasa mzima jinsi ilivyokuwa katika siku hiyo.
Alisema kuwa baada ya kukaa na wananchi wenzake na kutafakari jambo hilo kwa muda mrefu huku visomo mbali mbali vikipitishwa, bila ya kufanikiwa kumpata mtu huyo, ndipo alipopata mawazo kutoka kwa mzungu raia wa Ujerumani aliyemtaja kwa jina Mr. Chadi.
Alifafanua kuwa mzungu huyo alitoa wazo hilo na ndipo wananchi hao walipoamua kuanzisha ulinzi, muda wote lakini kwa kipindi hicho chote hawakuweza kumkamata, huku vitendo hivyo vikizidi kushamiri huku wakitumia pesa nyingi kwa kufanya dawa.
''Kila siku tumekuwa tukikesha hapa skuli lakini mara tu tunapoondoka basi vitendo hivyo vinafanywa, tena wakati mwengine mchana utakuta kinyesi kinarushwa''alisema.
Akieleza kuwa usiku wa kuamkia Jumanne wakati wakijitayarisha kutoka majira ya saa 11: 45 alfajiri, walimkuta kijana huyo akiwa anatembea nyuma ya majengo ya skuli, akiwa na mfuko wa plastic mkononi.
Alieleza kuwa baada ya kumhoji kwa muda mrefu ndipo kijana hayo alijulikana kwa jina la Kassim Ali Ame, mwenye umri wa miaka 13 mkaazi wa Muungoni mwanafunzi wa darasa la tano skuli ya Muungoni alieleza jinsi alivyokuwa akishiriki vitendo hivyo.
Alisema kuwa yeye alikuwa akitumwa na bibi mmoja aliyemataja kwa jina la Fatuma Kitanzi Mtaji (65), mkaazi wa Muungoni uwandani ili afanye kazi hiyo, akiwa na wenzake 7 wakifanya kazi hiyo huku wakipishana zamu.
Kijana huyo alieleza kuwa walikuwa wanafanya kazi hiyo kwa nyakati tofauti, ambapo wakati mwengine walikuwa wanaenda usiku wa manane kupaka kinyesi hicho, huku wakiwa wamefuatana na mtu mmoja ambaye yeye mwenyewe alidai kuwa hamfahamu,lakini alikuwa ni mrefu sana na mwenye upara.
Alisema kuwa wakati alipokuwa akifanya kazi hiyo yeye na wenzake walikuwa wakipewa pesa ambazo alizitaja kati ya kiasi cha shilingi 5000 mpaka 3000, ambazo alikuwa akitumia wakati anapokwenda skuli.
Alieleza kuwa wakati kupaka kinyesi hicho hutumia mikono kupaka na mengine hurusha kupitia madirisha ya skuli, bila ya kuonekana na mtu yoyote kwa kipndi hicho.
Mapema mwalimu mkuu wa skuli hiyo Mrisho Pandu Ali alisema kuwa kukamatwa kwa mtu huyo kutaleta afueni, kwani walikuwa wanaathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na jambo hilo.
Alisema kuwa walilazimika kuwafungia skuli wanafunzi wa madarasa ya chini kutokana na kadhia hiyo, iliyokuwa imeshamiri skuli hapo na kulazimika kufupisha silibasi yao.
Kwa upande wake bibi huyo ambaye anashutumiwa kuwatumia vijana hao wadogo kufaya vitendo hivyo vya kishirikina,imebainika kuwa anafanya hivyo kutokana na skuli hiyo kujengwa katika eneo lake.
Wananchi wa Muungoni walisoma halbadiri kadhaa na visomo vya kila kumuoamb Mwenyezi Mungu awaondoshee balaa hilo lakini kila kisomo kikipigwa ndipo kinyesi hicho kinapozidi.

No comments:

Post a Comment