Thursday 23 June 2011

POLISI NETIBOLI YAENDELEZA MKONG'OTO

Polisi netiboli yaendeleza mkong'oto

Na Mwajuma Juma
TIMU ya netiboli ya Jeshi la Polisi wanaume, imeendelea kutamba kwenye ligi kanda ya Unguja, kwa kuifunga Jitegemee mabao 63-25 kwenye uwanja wa Gymkhana.
Ikiwatumia wafungaji wake Amiri Muhidin na Ali Hamad, Polisi ilitawala mchezo na kuwaweka roho juu wachezaji wa Jitegemee, ambapo hadi mapumziko walikuwa mbele kwa mabao 30-15.
Katika mchezo wake wa kwanza wa ligi hiyo, maafande hao waliibwaga Msambweni kwa mabao 45-26.
Ligi hiyo inayoshirikisha timu 15 zikiwemo nane za wanawake na saba za wanaume, inatarajiwa kuendelea tena leo uwanjani hapo kwa michezo miwili kati ya Msambweni na Pangawe, na baadae Ikulu na Zimamoto.

No comments:

Post a Comment