Tuesday 21 June 2011

SUZA YAPATA BARAZA JIPYA

SUZA yapata Baraza jipya

Na Mwandishi wetu
WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ramadhan Abdulla Shaaban
amewateuwa wajumbe 1 wapya wa Baraza la Chuo Kikuu cha
Taifa cha Zanzibar (SUZA).
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali, Mwanaidi Saleh Abdulla, Waziri Shaaban
amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa sheria namba 8 ya mwaka 1999 ya Chuo
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kifungu cha 12(d).
Walioteuliwa kuwa wajumbe wa Baraza hilo ni Said Mohammed Said
Mwakilishi kutoka Baraza la Wawakilishi, Dk. Narman Saleh Jiddawi
kutoka Taasisi ya Sayansi ya Bahari ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Simai Mohammed Said ambae ni mfanyabiashara, Amina Khamis Shaaban Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar,
Khamis Mussa Omar Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na
Mipango ya Maendeleo na Mwanaidi Saleh Abdulla Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali.
Wengine ni Dk. Zakia Mohamed Abubakar, kutoka SUZA, Mmanga Mjengo Mjawiri kutoka SUZA, Maulid Omar Haji kutoka SUZA, Profesa Mustafa Roshash
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar na Mtumwa Ali Ameir
Mwenyekiti wa Serikali ya Wanafunzi SUZA.
Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa, Hassan Nassor Moyo ataendelea kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo.
Uteuzi huo umeanza tarehe 15 Juni mwaka huu.

No comments:

Post a Comment