Monday 25 April 2011

CHUMBAGENI WAHITAJI MSAADA UJENZI MADRASA.

Chumbageni wahitaji msaada ujenzi madrasa

Na Haji Nassor ZJMMC
ZAIDI ya shilingi milion tano zinahitajika kumalizia ujenzi wa Madrasatul Anuwar ilioko Chumbageni wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini huko Mwalimu Mkuu wa Madrasa hiyo Omar Juma Ussi, alisema fedha hizo wanatarajia kuziomba kwa wafadhili mbali mbali ikiwa ni pamoja na wazaliwa wa Chumbageni, wahisani, wafanyabiashara kutoka kwa wananchi.
Alisema kwa sasa ujenzi wa madrasa hiyo ambao uko katika hatua ya msingi tayari wameshatumia shilingi 950,000, ambapo ni michango kutoka kwa wazazi, waalimu, wanafunzi, pamoja na wahisani mbali mbali.
Mwalimu Omar alieleza waliamua kuanzisha ujenzi huo wa kudumu kutokana na eneo husika kuwa na ukosefu madrasa kwa ajili kuwasomeshea wanafunzi, ambapo kwa sasa wanatumia baraza ya nyumba ya mwalimu huyo.
“Kwa kweli kwa sasa tunalazimika kusomo tu kwa siku hizi za jua kazi na zile siku za mvua hulazimika kukatisha masomo jambo ambalo huwapotezea muda’’, alifafanua.
Alifafanua kua mara tu madrasa hiyo itakapomalizika ambayo imeanza miaka miwili iliopita, itakapomalizika itakua na uwezo wa kusomewa na wanafunzi zaidi ya 200 kwa wakati mmoja.
Akizungumzia juu ya ushirikiano uliopo baina yake na wazazi wa wenye watoto katika madras hiyo , alieleza sio mzuri sana kwa vile baadhi ya wazazi ,wamekua wagumu kufika wakati wanapoitwa kwa ajili ya mikutano .
Katika hatua nyengine Mwalimu Mkuu huyo wa Madrsatul Anuwar ya Chumbageni Mkoani, Omar Juma Ussi alieleza kua wakati umefika sasa kwa wazazi na walezi kufuatilia kwa karibu neyenendo za watoto wao.

No comments:

Post a Comment