Monday 25 April 2011

KINAMAMA WASHAJIISHWA KUWANIA UONGOZI.

Kinamama washajiishwa kuwania uongozi

Na Aboud Mahmoud
AKINA mama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wametakiwa kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hivho wakati wa uchaguzi utakapowadia hapo mwakani.
Mbunge wa Viti maalum wanawake CCM, Faharia Shomari aliwakati alipokuwa akizungumza na akina mama wa Umoja wa Wanawake wa Wilaya ya Mjini 'UWAWIMI SACCOS' huko Miembeni.
Faharia alisema umefika wakati wa akina mama kujitosa kuwania nafasi za uongozi wa chama hicho ili waweze kutoa mchango wao katika kukiimarisha na kuwatumikia wananchi kwa ujumla.
Aidha alisema mbali na kuwania nafasi za uongozi wa chama, lakini pia aliwataka akina mama kufanya maandalizi ya kujitokeza kuwania nfasi za juu kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
"Napenda kukushaurini akina mama wenzangu kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi za uongozi katika chama chetu na pia kujitokeza kuwania nafasi za juu katika uchaguzi mkuu",alisema.
Katika mkutano huo aliokutana na akina mama wa UWAWIM, Mbunge huyo alichangia shilingi milioni moja kwa ajili ya kuongezea mfuko wa Saccos ya akina mama hao.
Mbunge huyo alimkabidhi fedha hizo Katibu wa Saccos hiyo,Salma Mohammed Seif na kusema kuwa hiyo ni ahadi yake aliyoitoa kwa akina mama wa UWAWIM.
Akitoa shukurani kwa Mbunge huyo,Mjumbe wa Saccos ya UWAWIM, Mtumwa Mussa Kibendera alimpongeza kwa msaada wake alioutoa na pia kuwataka akina mama wenzake kufuata maneno ya Mbunge huyo.
Aidha mjumbe huyo aliwataka akina mama hao kudumisha umoja wao na mapenzi ambayo yatasaidia kukiinua zaidi chama na kujiletea maendeleo binafisi.

No comments:

Post a Comment