Monday 25 April 2011

UJAMAA YAFANYA MAUAJI.

Ujamaa yafanya mauaji

Na Suleiman Bangaya

KATIKA ligi ya soka daraja la pili Wilaya ya Mjini inayopendelea kupamba moto kwenye viwanaj mbalimbali, timu ya Ujamaa juzi ilifundisha soka G. S. United kwa kuichapa magoli 6-0.
Katika mchezo mwengine wa michuano hiyo, Bondeni ikawa uchochoro mbele ya Kilimani ilipokubali kichapo cha mabao 2-0.
Na katika matokeo ya mashindano ya Kombe la 'May Day', maveterani wa KMKM wakala sahani moja kwa kufungana bao 1-1 na Ardhi.
Bao la KMKM lilipachikwa nyavuni na Ibrahim Said katika dakika ya nne, huku lile la Ardhi likifungwa na Abdulrahim mnamo dakika ya 18.

No comments:

Post a Comment