Friday 29 April 2011

MIFUKO YA PLASTIKI IMEJAA MJINI

Mifuko ya plastiki imejaa Mjini

Na Halima Abdalla
ZAIDI ya kilo 1,500 za mifuko ya plastiki imekamatwa katika maeneo mbali mbali ya masoko Mkoa wa Mjini Magharibi.
Hayo yameelezwa na Afisa elimu ya Mazingira, Hamza Rijaal, kutoka Idara ya Mazingira alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu huko ofisini kwake Maruhubi.
Hamza alisema mifuko hiyo imekamatwa katika masoko mbali mbali ikiwemo soko la Mwanakwerekwe, Malindi, Darajani, Mombasa, Mikunguni na kwa Haji tumbo.
Alieleza kuwa lengo la kuikamata mifuko hiyo ni kuufanya Mji kuwa katika haiba ya kupendeza na muonekano na haiba ya kupendeza.
Alisema kuwa baada ya kukamatwa kwa mifuko hiyo Idara ya mazingira iliamua kwenda kuichoma moto katika eneo la Maruhubi ili moshi wake usiweze kuleta madhara wa wananchi waliokatika maeneo ya karibu.
Alifahamisha kuwa kabla ya kuipeleka Maruhubi walikuwa na wazo la kutaka kuipeleka Dar esSaalam kwenda kuichoma moto katika tanuri kubwa lililopo huko.
Aidha alisema mtu yeyote atakaekamatwa na mfuko wa plastiki japo mmoja atatakiwa kulipa faini kuanzia 500,000 mpaka milioni 1500,000 au kwenda jela miezi 6 au kutumikia adhabu zote mbili.
Alisema kuwa Idara yao sasa imejipangia kwa kila siku asubuhi kufanya opresheni kwa kupita katika maeneo mbali mbali ya masoko kukamata mifuko ya plastiki ili kuepusha kueneo mifuko hiyo katika maeneo ya Mji hasa katika kipindui hiki cha masika ili kuepusha maradhi ambayo yanatokana na uchafu.
Sambamba na hayo Afisa huyo alitoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuacha kutumia na kuuza mifuko ya plastiki ili kuepusha matatizo yasiokuwa na lazima.

No comments:

Post a Comment