Saturday 30 April 2011

HAROUN ATAKA MAONESHO YASHIRIKISHE TAASISI ZA NJE

Haroun ataka maonesho yashirikishe taasisi za nje

Na Ali Mohamed, Maelezo
WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman amesema shirikisho la vyama vya Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC), kuzishirikisha taasisi za nchi za Tanzania Bara na Afrika Mashariki kwenye maonesho ya ‘May Day’.
Akizungumza na vyama vya ushirika, taasisi za umma na za binafsi na wananchi walioshiriki katika maonyesho ya biashara na huduma katika viwanaja vya Amani nje, alisema kufanya hivyo kutakuza soko la nje na kuingeza pato la taifa.
Alisema lengo la maonyesho hayo ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza Zanzibar ni kutangaza bidhaa na huduma zinazopatikana Zanzibar, hivyo taasisi za umma na binafsi pamoja na vyama vya ushirika ni vyema wakatumia fursa hiyo kujutangaza kibishara.
Alisema mapungufu yaliyojitokeza yawe changamoto kwa waandaji na kuyafanikisha maonyesho yajayo ikiwemo kuzishirikisha taasisi na vyama vya ushirika vingi zaidi vya ndani na nje ambapo kuahidi serikali kuunga mkono.
"Tuonyeshe wananchi shughuli, huduma na majukumu yetu ya kazi tunayoyatekeleza katika sehemu mbali mbali za kazi ikiwa ofisini, viwandani na kwengineko na maonyesho haya yawe sehemu ya kuona na kukunua bidhaa na huduma na kupata kipato cha kuendeleza maisha yetu",alifahamisha waziri Haroun.
Alisema serikali inafahamu kutokuwepo eneo maaluma la maonyesho ya biashara na huduma ambayo hiyo ni changamoto na aliahidi kuwa itafanya kila liwezekanalo kutafuta sehemu maalumu ya maonyesho hayo ambayo yatakuwa yanafanyika kila mwaka ikiwa ni miongoni mwa ratiba za maazimisha ya siku ya wafanyakazi May Day.
Aidha Waziri Haroun alisema kuwa Zanzibar kama nchi nyengine lipo tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana ambapo serikali imedhamiria kupunguza tatizo hilo kwa kujenga vituo vya kutoa taaluma kwa vijana, (skills Development Cetre) kuunda kamati za ajira katika wilaya zote kwa lengo la kuzalisha ajira kwa vijana.
Alisema maonyesho hayo pia yalenge kuwashajihisha vijana kubuni njia za biashara na miradi amabayo itawasaidia kujiaajiri, kuwaajiri wenzao na kutengeza nafasi za ajira.
Waziri Haroun alitoa ushauri kwa wafanyakazi kujiunga na vayama vya wafanyakazi na shirikisho la wafanyakzi ili kuongeza umoja mshikamano na kutetea maslahi yao katika mazingira ya kazi.
Kwa niaba ya wafanyakazi katibu wa shirikisho hilo la Wafanyakazi Zanzibar ZATUC, Khamis Mwinyi Mohammed alisema wafanyakazi wanahaki ya kushirikishwa katika mambo yanayowahusu amabayo ni kauli mbuyu ya maazimisho ya siku ya wafanyakazi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment