Saturday 30 April 2011

MAKAMPUNI YA UTURUKI KUKARABATI VIWANJA VYA NDEGE

Makampuni ya Uturuki kukarabati viwanja vya ndege

Na Rajab Mkasaba,
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imetiliana saini makubaliano ya maelewano na makampuni matatu makubwa ya Uturuki ambayo yatashughulikia ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vya Unguja na Pemba.
Makubaliano hayo yalisaini jana katika Hoteli ya Sheraton mjini Ankara Uturuki, ambapo kwa upande wa Zazibar iliwakilishwa na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo Omar Yussuf Mzee.
Akizungumza kabla ya kutiwa saini makubaliano hayo, Mzee alsema kuwa mradi huo ambao umekisiwa kuharimu kiasi cha dola za Marekani milioni 40, utahusisha matengenezo makubwa katika uwanja wa ndege wakimaifa wa Zanzibar unaotumika hivi sasa kwa ujenzi wa jengo la abiria.
Aidha, alisema kuwa kwa upande wa uwanja wa ndege wa Pemba, kampuni hizo zitaujenga uwanja huo pamoja na kutiwa taa ili kuwezesha ndege kuweza kutua usiku na mchana.
Mzee alisema kuwa serikali inaendelea na hatua kukamilisha mkataba kwa ajili ya mradi huo ili ikiwezekana utekelezaji wake uanze katika mwaka ujao wa fedha.
Nae mwakilishi wa Makampuni hayo ya YDA-ORIZZONTE-SARAYLI (YDA –ORSA) Huseyin Arslawa alisema kuwa hatua hiyo ni mwanzo katika utekelezaji wa miradi mengine inayokusudiwa kuekezwa na makampuni hayo kwa hapa Zanzibar.
Alisemasambamba na utekelezaji wa mradi huo kampuni hiyo itajenga hoteli ya kisasa kisiwani Pemba ambayo inatarajiwa kuanza kazi rasmi mara tu baada yakukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo wa ndege.
Pamoja na hayo alisema kuwa Uturuki imeamua kwa dhati kuelekeza nguvu zake za uwekezaji katika nchi za Afrika hasa katika maeneo ambayo amani na utulivu vimetawala ikiwemo Zanzibar.

No comments:

Post a Comment