Saturday 30 April 2011

KITOPE KUANZISHA ULINZI SHIRIKISHI

Kitope kuanzisha ulinzi shirikishi

Na Zainab Ali, MCC
WANANCHI wa shehia ya Kitope wapo mbioni kushirikiana kuanzisha Ulinzi shirikishi kutokana na kukithiri vitendo vya uhalifu katika shehia yao.
Sheha wa shehia ya Kitope, Bakari Khamis Simai alieleza hayo alipokuwa akizungumza na mwaandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Kitope wilaya ya Kaskazini ‘B’.
Sheha huyo alifahamisha kuwa ulinzi huo utasaidia kupiga vita vitendo viovu vikiwemo wizi wa mifugo, na mazao katika mashamba wakilima wa kijiji hicho.
Sambamba na hayo jeshi la polisi likishirikiana na wananchi wamesema mtu atakayekamatwa akijihusishwa na uhalifu ikiwemo wizi atachukuliwa hatua za kisheria.
Vile vile Bakari Khamis alisema wananchi wake wajitokeze kwa wingi ili kulisawazisha suala hili kwapamoja kuondokana na udhalilishaji wa kijamii.
Hata hivyo aliwaomba wananchi hao wawe wastahamilivu sana na usumbufu utakaotokezea kwani wapo mbioni kulifanyia matayarisho ili kudumisha usalama na amani katika shehia yao.

No comments:

Post a Comment