Monday 25 April 2011

WAUMINI WA KIKIRISTO WAASWA KUENDELEZA IBADA.

Waumini wa kikiristo waaswa kuendeleza ibada

Na John Mpiga Picha
WAUMINI wa dini ya Kikristo hapa wametakiwa kuendeleza ibada za kumkumbuka Mungu, sambamba na kujiepusha na makatazo kwenye mafundisho ya dini hiyo.
Paroko wa Parokia ya Kitope, Faida Shio alieleza hayo kwenye mahubiri ya ibada ya Pasaka iliyofanyika kwenye kanisa hilo, lilioko Kitope Wilaya ya Kaskazini ‘B’.
Alisema dunia imekubwa na matatizo mengi na kwamba njia ya kuepukana na matatizo hayo ni kwa waumini wadini kuongeza kufanya ibada na matendo mema kwa nia ya kumuomba Mungu muumba.
Shio alisema Mungu hapendelei viumbe wake kupata matatizo yakiwemo maradhi pamoja na majanga mbalimbali yanayotokea ulimwenguni na akhera na kuwa mwepesi zaidi kuwaepusha na matatizo hayo waja wake wanapomuomba katika ibada.
Sambamba na hilo kiongozi huyo wa kanisa aliwahimiza waumini hao kuwa na ushikamano kati yao na waumini wa dini nyengine katika kuala zima la kuleta maendeleo ya nchi.
"Ubaguzi wa dini tuondosheni katika nchi na kuwa sote kitu kimoja katika kuendeleza kuijenga nchi yetu ambayo inahitaji kuwa na mabadiliko yatokanayo kwa nguvu yetu moja,"alisisitiza kiongozi huyo.
Alisema suala la maendeleo ya nchi linamuhusu kila mwananchi bila ya kujali dini wala kabila lake ambapo aliwataka kushirikiana kikamilifu katika masuala ya ujenzi wa taifa ikiwa pamoja na kujenga shule pamoja na vituo vya afya.
Katika kusherehekea sikukuu hiyo ya Pasaka waumini kadhaa wa Kikristo, jana walijazana katika makanisa mbali mbali kwa kuifanya ibada za Pasaka.
Waumini wa dini hiyo wanaadhimisha kukumbuka mateso na kufufuka kwa kiongozi wao Yesu Kristo.

No comments:

Post a Comment