Monday 25 April 2011

TUMAINI MICHEZO KUDUMISHA UDUG, MUUNGANO

'Tumieni michezo kudumisha udugu, muungano'

Na Mwajuma Juma

WANAMICHEZO wa afisi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar, wameshauriwa kuitumia michezo kama njia ya kujenga ushirikiano, upendo, udugu pampoja na kudumisha muungano wa Tanganyika na Zanzbar.
Ushauri huo umetolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar Fatma Mohammed Said, katika hafla ya uzinduzi wa tamasha la michezo kwa afisi hizo, lililofanyika viwanja vya Chuo cha Afya Mbweni.
Amesema kimsingi michezo ni miongoni mwa njia za kuleta maelewano na sio ugomvi, na kuwataka waichukulie kwa malengo hayo na si kwa ajili ya kupata kikombe au zawadi kutokana na michezo hiyo.
Nae Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Selina Lymo, amewataka wanamichezo hao kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za michezo ili waendelee kujenga ushirikiano uliopo miongoni mwao.
Mapema Katibu Msaidizi wa timu ya Soka ya ukaguzi alisema kuwa umoja na mshikamano walionao baina ya taasisi mbili hizo utazidi kuendelezwa ili kuwa mfano mzuri kwa wafanyakazi watakaofuatia baada yao.
Katika uzinduzi huo uliotanguliwa na maandamano ya wanamichezo, timu ya Soka ya Ukaguzi ya Zanzibar ilishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya wageni wao Ukaguzi kutoka Tanzania Bara, mabao yaliyofungwa na Haji Mohammed na Hakim Khamis.

No comments:

Post a Comment