Monday 25 April 2011

WAATHIRIKA MAFURIKO MOROGORO WAOMBA KUSAIDIWA.

Waathirika mafuriko Morogoro waomba kusaidiwa

Na Nalengo Daniel, Morogoro
SERIKALI imeombwa na wananchi waliokumbwa na mafuriko wilayani Kilosa mkoni hapa, kufanya ukarabati wa eneo lilokumbwa na mafuriko wilayani humo ili waweze kurudi katika maeneo yao na kuishi maisha ya kawaida.
Hayo yalibainishwa na wananchi hao kwenye mkutano wa kuunda kamati ya nguvu mji, ikiwa ni lengo la kuwasilisha malalamiko yao kwa viongozi husika.
Akizungumza kwenye mkutano huo Mwenyekiti wa kamati hiyo Nchimbi Nackam, alisema wameamua kuiomba serikali baada ya kuona viongozi husika kulisahau eneo hilo katika kulirudisha katika hadhi yake kama ilivyo kuwa zamani.
Nchimbi alisema kwa sasa serikali haina budi kupanga mipango ya kuboresha mji huo hasa, baada ya kujengwa kwa kingo za uzio wa kuzuia mto mkondoa, ili usipoteze tena mwelekeo ambao ndio chanzo kikubwa katika kuleta mafuriko eneo hilo.
Alisema wameridhishwa na serikali katika kudhibiti yasitokee tena mafuriko katika eneo hilo, pamoja na JWTZ kuendelea kujenga tuta katika mto huo, lakini pia wameridhishwa na ujenzi wa bwala la kidete ambalo linapunguza kasi ya maji yanapotiririka.
Mwenyekiti huyo alisema mbali na baadhi ya nyumba za watu kubomoka katika mafuriko hayo pia huduma za kijamii zimeathirika, ikiwa ni pamoja na Machinjio,Shule ya msingi mkondoa, ofisi ya CCM, Misikiti,soko,Miundombinu ya barabara na mifereji nayo iliharibika.
Alisema kuwa pamoja na Mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Fedha Mustapha Mkulo kutoa msaada wa ujenzi wa msikiti katika eneo hilo, lakini selikali inatakiwa kufanya haraka kurudisha mji katika hali yake kwa kujenga huduma hizo za kijamii.
Kwa upande wao wakazi wa mji huo wakiongea kwa nyakati tofauti katika mkutano huo Masoud Bombolage,Haji Nasoro,Kasamila Kibwana, Rebeka Salum,Amina Khasim,na Ally Waziri wameiomba selikali kutimiza ahadi zake kwa wahathirika wa mafuriko hayo, ikiwa ni pamoja na kupewa viwanja waliohaidiwa sambamba na kuboreshwa kwa mji huo, ili baadhi yao wanaokaa katika makambi waweze kurudi katika maisha yao ya kila siku.
Wananchi hao walisema maeneo ambayo yaliathirika na mafuriko hayo ambayo yanatakiwa kuangaliwa na kurudishwa katika hadhi yake ni pamoja na Mbumi B, Kasiki,Mbumi A, Behewa,kibaoni,Kondoa,Mbwamaji,Masenze na kichangani
Mwishoni mwa mwaka 2009 Wilaya ya Kilosa ilikumbwa na mafuriko ambapo watu watu wawili walipoteza maisha na nyumba kadhaa kubomoka huku wananachi 4610 wakikosa makazi.

No comments:

Post a Comment