Saturday 30 April 2011

WANAFUNZI WASUFA ZIARANI KILIMANJARO , MANYARA.

Wanafunzi wa Sufa ziarani Kilimanjaro, Manyara

Na Ameir Khalid
JUMLA wanafunzi na walimu 55 wa skuli ya sekondari ya Sufa iliopo Tomondo wilaya ya Magharibi wako kwenye ziara ya kimasomo katika Mikoa ya Kilimanjaro, Manyara na Arusha kwa lengo la kujifunza.
Walisema kuwa katika ziara hiyo ya wiki moja ambayo walitembelea sehemu tofauti imewajengea uelewa mzuri, kwa kufahamu Geografia ya Mikoa hiyo ambao utaweza kuwasaidia kwenye kujibu mtihani wao mwishoni mwa mwaka.
Katika ziara hiyo wanafunzi hao ni wenyeji wa skuli ya Ufundi ya Moshi iliyopo wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro, wakiwa katika Mkoa wa Kilimanjaro watapata fursa ya kupanda mlima mkubwa kuliko yote barani Afrika, Kilimanjoro.
Pamoja na kutembelea maporomoko ya maji katika kijiji cha Materumi yanayotirikia katika ziwa la nyumba ya Mungu ambalo linasaidia kutoa kiwango cha umeme wa megawati 8 kwenye gridi ya taifa.
Katika Mkoa wa Manyara walitembea katika msitu wa hifadhi wa Tarangere ambapo walipata kuona aina mbali mbali za wanyama, sambamba na kujuwa historia kamili ya hifadhi hiyo na aina ya wanyama waliomo katika hifadhi.
Wanafunzi hao walimalizia ziara yao kwa kutembea katika Mkoa wa Arusha na kupata kuona hifadhi ya nyoka, sambamba na kupata kufahamishwa historia ya kabila la wamasai ambalo bado linaonekana kuwa na nguvu pamoja na kuvishwa mavazi ya kabila hilo.
Akizungumzia na mwandishi wa habari hizi mwalimu mkuu wa skuli ya Sufa, Abubakar Suleiman alisema kuwa ziara hiyo ni moja ya mipango ya skuli yake, ambayo kila baada ya muda huwatembeza wanafunzi sehemu tofauti kwa lengo la kujifunza zaidi.
Alisema kuwa ziara kama hizo ni mzuri katika kuzidisha ufahamu wa wanafunzi hivyo skuli itaziendelezai kwa manufaa ya wanafunzi wake katika kufahamu mambo tofauti juu ya masomo yao ya darasani.

No comments:

Post a Comment