Friday 29 April 2011

WANAOWATUHUMU UFISADI ROSTAM,LOWASA WAKATHIBITISHE MAHAKAMANI.

Wanaowatuhumu ufisadi Rostam, Lowasa wakathibitishe mahakamani

Na Nalengo Daniel, Morogoro
KADA wa Chama cha Mapinduzi (CCM), David Msuya amewataka wanaodai kuwa mbunge wa jimbo la Igunga Rostam Azizi, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Monduli Edward Lowasa kuwa ni mafisadi wakathibitishe mahakamani badala ya kuendeleza fitina.
Kada huyo alisema hayo mjini hapa wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ,na kwamba serikali haijawahi kutoa tamko juu ya watuhumiwa hao, na shutuma ya ufisadi inayozungumzwa na baadhi ya watu na kwamba hayo ni majungu yanayotengezezwa na watu wachache.
Alisema kuwa wanaodai kuwa Rostam Azizi na Lowasa ni wafisadi anatakiwa kwenda mahakamni wakiwa na ushahidi wa kutosha na kueleza hizo fedha ziliibiwa wapi na kwa ushahidi upi ili wananchi wawelewe badala ya kuongea bila uthibitisho.
“Hili suali linashangaza kwa nini chama kiseme serikali ikae kimya? na kama ni kweli ni mafisadi, kwa nini serikali isitoe tamko”, alihoji kada huyo.
Msuya alisema kuwa ni nani wa kumwamini ndani ya Chama na kwamba watu wanaosema kuwa watu hao ni mafisadi wanatakiwa kutambua kuwa hao ni watumishi wa serikali kupitia vyama vyao.
Aliwataka watu wanaowanyoshea vidole, kuacha tabia hiyo kwa kuwa kufanya hivyo ni kumdhalilisha mtu bila ushahidi na kwamba kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Aidha kada huyo alisema kuwa Mwananchama wa CCM ikiwa amekosea huitwa kwenye kamati ya maadili na kuonywa na masuala hayo hutakiwa kuishia ndani ya chama.
Alisema anashangazwa na tabia ya baadhi ya viongozi ‘CCM’ ambao wamekuwa wakitoa taarifa za siri zinazotakiwa kubaki ndani ya chama na kuhoji kuwa huo ndiyo utaratibu wa chama?
Hata hivyo kada huyo amesema kuwa pamoja na kutishwa na badhi ya viongozi kutokana na msimamo wake, hataacha kuendelea kuwatetea wasio na makosa, na kwamba kwenye ukweli ataongea.

No comments:

Post a Comment