Saturday 30 April 2011

TUMBATU UVUVINI WATAKA BWANASHAMBA

Tumbatu Uvuvini wataka mbwanashamba

Na Biubwa Hafidh MCC
WANANCHI wa shehia ya Tumbatu Uvivini wameiomba serekali kipitia wizara ya Kilimo na Maliasili, kuwapatia mabwanashamba ili waweze kujiendeleza katika shughuli zao za kilimo.
Ushauri huo umetolewa na wananchiwa shehia hiyo walipokuwa wakizungumza na wandishi wa habari hizi huko wilaya ndogo Tumbatu.
Walisema kuwa kutokana na ukosefu wa wataalam wanaotoa elimu upandaji wa mimea, ndio chanzo kinachorejesha nyuma shughuli za kilimo katika kisiwa hicho.
Hali hiyo inatokana na hali halisi ya kisiwa hicho kuzunguukwa na mawe jambo ambalo husababisha kutoimarika kwa mazao wanayozalisha kwa ajili ya chakula ili kukabiliana na tatizo la njaa ambalo huwaathiri wakaazi wa kisiwa hiucho katika kipindi cha ukame.
Miongoni mwa mazao wanayozalishwa na wakazi wakisiwa hicho ni pamoja na mihogo,mahindi choroko,mtama na viaazi vitamu.
Aidha walisema kuwa pindipo serekali itakapowapatia wataalam utawawezesha wananchi hao kujiimarisha kiuchumi na kiondokana na utegemezi.
Nae sheha wa sheha wa shehia hiyo Nyange Vuai Nyange alisema kuwa mbegu ni kikwazo kikubwa kinacho wakabili wananchiwa eneo hilo hawana uwezo kununua mbegu wanazozikitaji katika misimu ya kilimo.
Hivyo aliiomba serekali kuwapatia mbegu za mazao mbalimbali ili waweze kuzalisha kama wanavyozalisha wananchi wa maeneo mbali mbali hapa nchini .

No comments:

Post a Comment