Monday 25 April 2011

UKOSEFU WA ELIMU WAKWAMISHA UCHANGIAJI WA DAMU.

Ukosefu wa elimu wakwamisha uchangiaji damu

Na Juma Haji, MCC
BENKI ya damu ya Zanzibar imesema ukosefu wa elimu kwa makundi hatarishi yamekuwa ni kikwanzo kinachochelewesha kufikia malengo ya kimaendeleo kwa benki hiyo.
Hayo yameelezwa na katibu Mkuu wa benki hiyo Bakari Hamadi Magarawa alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Amani mjini hapa.
Alisema maendeleo katika benki hiyo yamekuwa ni madogo kutokana na vijana wengi kujiingiza katika makundi hatarishi.
Alisema kuwa kukosekana kwa mchango wa vijana hao kwenda kutoa damu kwa hiari imekuwa ni sababu ya kuzorotesha kwa maendeleo ya huduma za benki hiyo.
Magarawa aliyataja makundi ya vijana kuwa ni wanaotumia dawa za kulevya na wanaojidunga sindano amabao pia wana mchango mkubwa kwa jamii kupitia benki hiyo.
Hata hivyo aliwataka wanawake wasiogope kuchangia damu kwa kisingizio cha kujulikana afya zao na wanajamii.
"Wanawake wengi wamekuwa wakiogopa kwenda kupima afya zao kwa kisingizio cha kujulikana na jamii utaona kwenye wanawake 50 wanakwenda 5 wamezidi 10", alisema mkuu huyo.
Nae mshiriki wa uchangiaji wa utoaji damu katika benki hiyo Abrahamani Salum, alipongeza huduma hizo zinazotolewa na kitengo hicho kwa kuwa bado zinalenga maisha ya binaadam.
Hata hivyo alisema kwa marayakwanza walikuwa na usiri kushiki katika zoezi hilol lakini sasa wameshajihishika juu ya umuhimu wahuduma hiyo.

No comments:

Post a Comment